Picha/ kwa hisani
Klabu ya Bandari imetoka sare ya kutokufungana na klabu ya Mathare United.
Mechi hiyo imesakatwa katika uwanja wa Kenyatta mjini Machakos.
Kabla ya Ngarambe hiyo mkufunzi wa Badari Ken Odhiambo aliambia vyombo vya habari kuwa walikuwa wanalenga kupata ushindi katika mechi hiyo.
Na matokeo haya klabu ya Bandari inaujumla wa pointi 24.
Kwa sasa Bandari wanajiandaa kwa ajili ya mechi ya nyumbani dhidi ya Posta. Mechi hiyo itachezwa tarehe 19 Mei.
Taarifa na Dominick Mwambui.
Viongozi wa kaunti ya Mombasa wakosoa kupunguzwa kwa mgao wa fedha
Baadhi ya viongozi wa kaunti ya Mombasa wameikosoa hatua ya serikali kuu kwa kupunguza mgao wa fedha wa bajeti ya mwaka wa 2019/2020 kwa kaunti hiyo kwa asilimia 12.
Uongozi duni watajwa kuwa chanzo cha kukosekana kwa maendeleo
Mwanaharakati wa masuala ya kisiasa mjini Mombasa Ali Mwatsahu amesema maeneo bunge ya kaunti ya Mombasa yamekosa kujiendeleza kimaendeleo kutokana na uongozi duni.