Wakiongozwa na Hassan Kombo Ismail wamesema kuwa visa vya unyanyasaji kwa mabaharia wa Kenya vimekithiri mno kwani wamesema mabaharia humu nchini hawathaminiwi kuliko wale wakigeni hatua anayoitaja kuvunja moyo za mabaharia.
Mabaharia hao aidha wameongezea kwamba licha ya wao kupeleka malalamishi yao kwa mamlaka hiyo hakuna hatua zozote zinachuliwa na kupelekea wengi wao kuishi bila ajira.
Taarifa na Hussein Mdune.
Viongozi wa kaunti ya Mombasa wakosoa kupunguzwa kwa mgao wa fedha
Baadhi ya viongozi wa kaunti ya Mombasa wameikosoa hatua ya serikali kuu kwa kupunguza mgao wa fedha wa bajeti ya mwaka wa 2019/2020 kwa kaunti hiyo kwa asilimia 12.
Uongozi duni watajwa kuwa chanzo cha kukosekana kwa maendeleo
Mwanaharakati wa masuala ya kisiasa mjini Mombasa Ali Mwatsahu amesema maeneo bunge ya kaunti ya Mombasa yamekosa kujiendeleza kimaendeleo kutokana na uongozi duni.