Zaidi ya magunia elfu 8 ya sukuri yanayokisiwa kuingizwa humu nchini kimagendo yameharibiwa katika bandari ya Mombasa.
Akiongoza hafla hiyo Waziri wa viwanda nchini Aden Mohammed amesema kuwa sukari hiyo yenye uzani wa tani 400 ilingizwa kinyume cha sheria kutoka nchini Brazil kupitia jina la kampuni moja ya Uganda ikiwa kwenye makasha 16.
Aden hata hivyo amesema wizara ya uchukuzi nchini haitaruhusu visa hivyo kundelezwa, akisema kuwa hatua hiyo ni kunyima taifa hili ushuru na kudidimiza uchumi.
Kwa upande wake waziri wa utalii nchini Najib Balala amesema kuharibiwa kwa sukari hiyo ni njia moja wapo ya kuimarisha viwango vya biashara humu nchini.
Taarifa na Hussein Mdune.
Viongozi wa kaunti ya Mombasa wakosoa kupunguzwa kwa mgao wa fedha
Baadhi ya viongozi wa kaunti ya Mombasa wameikosoa hatua ya serikali kuu kwa kupunguza mgao wa fedha wa bajeti ya mwaka wa 2019/2020 kwa kaunti hiyo kwa asilimia 12.
Uongozi duni watajwa kuwa chanzo cha kukosekana kwa maendeleo
Mwanaharakati wa masuala ya kisiasa mjini Mombasa Ali Mwatsahu amesema maeneo bunge ya kaunti ya Mombasa yamekosa kujiendeleza kimaendeleo kutokana na uongozi duni.