Mbunge wa Ganze Teddy Mwambire ameonya vijana na wanawake wanaojiingiza kwenye uhusianao wa kimapenzi na watoto wa shule ya Jila eneo la Bamba kaunti ya Kilifi kwamba watachukuliwa hatua za kisheria.
Teddy amesema kuwa visa kadhaa vimeripotiwa vya akina mama na vijana kuwaeka kinyumba wanafunzi wa shule hio kwa kisingizo kwamba wanawapa hifadhi.
Mbunge huyo wa Ganze amesema kuwa ukosefu wa mabweni katika shule hiyo na mahitaji mengine muhimu ya wanafunzi hasa wakike imechangia pakubwa kushuhudiwa kwa visa hivyo.
Taarifa na Marieta Anzazi.
Viongozi wa kaunti ya Mombasa wakosoa kupunguzwa kwa mgao wa fedha
Baadhi ya viongozi wa kaunti ya Mombasa wameikosoa hatua ya serikali kuu kwa kupunguza mgao wa fedha wa bajeti ya mwaka wa 2019/2020 kwa kaunti hiyo kwa asilimia 12.
Uongozi duni watajwa kuwa chanzo cha kukosekana kwa maendeleo
Mwanaharakati wa masuala ya kisiasa mjini Mombasa Ali Mwatsahu amesema maeneo bunge ya kaunti ya Mombasa yamekosa kujiendeleza kimaendeleo kutokana na uongozi duni.