Mazingira duni baharini na katika fuo za bahari Mombasa unahofiwa kuwasababisha watalii wengi kutozuru kaunti ya Mombasa.
Kwa mujibu wa Janet Morobi mshikadau katika sekta ya utalii Pwani, ni vyema kwa serikali ya kaunti ya Mombasa kulipa kipaumbele swala la usafi wa bahari ili kuimarisha viwango vya utalii.
Aidha ameitolea mwito mamlaka ya bandari nchini KPA kuzingatia usafi wa baharini ili kuimarisha kiwango cha watalii wanaozuru Pwani akisema watalii wengi kwa sasa wanazuru zaidi Pwani kusini kutokana na uwepo wa bahari na fuo safi eneo hilo.
Amehimiza kuidhinishwa kwa mpango wa kutumia vijana kusafisha bahari na mazingira ya bahari ili kuweka mazingira bora kwa watalii.
Taarifa na Hussein Mdune.
Viongozi wa kaunti ya Mombasa wakosoa kupunguzwa kwa mgao wa fedha
Baadhi ya viongozi wa kaunti ya Mombasa wameikosoa hatua ya serikali kuu kwa kupunguza mgao wa fedha wa bajeti ya mwaka wa 2019/2020 kwa kaunti hiyo kwa asilimia 12.
Uongozi duni watajwa kuwa chanzo cha kukosekana kwa maendeleo
Mwanaharakati wa masuala ya kisiasa mjini Mombasa Ali Mwatsahu amesema maeneo bunge ya kaunti ya Mombasa yamekosa kujiendeleza kimaendeleo kutokana na uongozi duni.