Muungano wa upinzani utawasilisha kesi mahakamani, kupinga matokeo ya uchaguzi mdogo wa ubunge wa Mbeere-Kazini

Kinara wa chama cha WIPER Kalonzo Musyoka ametangaza kwamba muungano wa upinzani utawasilisha kesi mahakamani, kupinga matokeo ya uchaguzi mdogo wa ubunge wa Mbeere-Kazini,kaunti ya Embu kwa misingi kwamba matokeo hayo yalikua na dosari. Akizungumza leo Jumapili Kalonzo amepuuzilia mbali kauli kwamba chama tawala cha UDA kilishinda ubunge wa Mbeere-kaskazini na ubunge wa Malava, akisema chama hicho kinatambua […]
Watatu wanaoshukiwa kuendeleza biashara haramu ya kusambaza pesa bandia katika kaunti ya Mombasa wanaswa

Maafisa wa polisi katika eneo la Diani kaunti ya Kwale wamewatia nguvuni watu watatu wanaoshukiwa kuendeleza biashara haramu ya kusambaza pesa bandia katika kaunti ya Mombasa na maeneo jirani. Kulingana na ripoti ya idara ya upelelezi wa jinai DCI, watatu hao Fadhili Lawrence, Atemba Lawrence na Electrine Okwako, wametiwa nguvuni wakiwa mafichoni huko Diani ambako […]
Maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani kuandaliwa Disemba Mosi.

Huku maadhimisho ya siku ya ukimwi duniani yakitarajiwa kuandaliwa kesho Disemba Mosi, katibu katika wizara ya afya Dkt Mary Muthoni amesema Kenya imepiga hatua katika mapambano dhidi ya HIV. Akizungumza na wanahabari Dkt Muthoni amesema katika miongo miwili iliyopita maambukizi ya HIV pamoja na vifo vinavyotokana na maambukizi ya virusi vya ukimwi yamepungua kwa kiwango […]