Vijana katika eneo bunge la Matuga kaunti ya Kwale watanufaika na ajira kuanzia mwaka ujao. Hii ni baada ya Mtengenezaji mkuu wa bidhaa za saruji na zege nchini Kenya, Bamburi Cement, kutia saini mkataba wa Uhandisi, Ununuzi, na Ujenzi wa shilingi bilioni 32 na kampuni ya Sinoma kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha klinka katika Matuga, Kaunti ya Kwale. Mbunge wa Matuga Kassim Tandaza amesema takriban vijana elfu 20 watanufaika na ajira.
Ujenzi wa kiwanda kipya cha klinka cha kisasa cha tani milioni 1.6 kwa mwaka, kinachojumuisha teknolojia za hali ya juu zisizo na kaboni ili kupunguza athari za mazingira, ni sehemu ya mkakati wa kampuni wa wa kuongeza mara mbili uwezo wake wa uzalishaji wa bidhaa bora za saruji na zege, ili kuwezesha maendeleo ya miundombinu ya Kenya na mabadiliko ya kiuchumi
Story by Correspondent



