Mashirika ya kijamii yakiongozwa na shirika la Samba Sports Youth Trust yameelezea hofu kufuatia ongezeko la visa vya ulawiti katika kaunti ya Kwale.
Akizungumza na wanahabari katika eneo la Kinondo Mkurugenzi wa shirika hilo Mohammed Mwachausa amesema hali hiyo inachangia ukiukaji mkubwa wa haki za watoto.
Kwa upande wake afisa wa tume ya kutetea haki za kibinadamu nchini KHRC Irene Soila ameitaka serikali kuangazia kwa kina suala hilo akisema tume hiyo inashirikiana na mashirika ya kijamii kaunti ya ya Kwale ili kutafuta suluhu la tatizo hilo.
Story by Janet Shume



