Mkuu wa majeshi nchini jenerali Charles Kahariri ametoa hakikisho kwamba idara ya ulinzi KDF imejikitika kuhakikisha utayari wa oparesheni, kuwapa kipaumbele maafisa wa idara hiyo na kuendeleza mikakati ya usalama wa taifa.
Jenerali Kahariri ametoa hakikisho hilo wakati wa ziara yake katika kambi ya jeshi la wanamaji ya Manda Bay kaunti ya Lamu, na vile vile amekutana na wanajeshi wa KDF wanaoendeleza oparesheni ya Amani Boni.
Kwenye maelezo yake wakati akihutubia maafisa hao Jenerali Kahariri amewapongeza wanajeshi hao akisema wameonyesha tajriba ya hali ya juu na kujitolea katika ulinzi wa taifa.
Mkuu huyo wa majeshi aidha amegusia mipango inayoendelezwa ya miradi ya kisasa jeshini, akisema wanalenga kuwekeza zaidi ili kuimarisha uwezo wa wanajeshi kufanikisha oparesheni za kiusalama.



