Mpiga Kura Awasilisha Kesi Akitaka Kusitishwa Maandalizi ya Uchaguzi wa 2027
Mpiga kura Benard Mwanzia amewasilisha kesi katika mahakama kuu,
akiitaka mahakama kusitisha maandalizi yote ya uchaguzi mkuu wa
mwaka 2027, yanayoendelezwa na tume huru ya uchaguzi na mipaka
nchini IEBC.
Katika kesi hiyo Mwanzia ameibua maswali ya kikatiba kuhusu uhalali
na uthabiti wa mfumo wa uchaguzi nchini, akiitaka mahakama
kuidhinisha kesi hiyo kuwa ya dharura.
Mwanzia katika kesi hiyo vile vile anaitaka mahakama kuzuia tume ya
IEBC,mawakala na wafanyikazi wa tume hiyo dhidi ya kutumia
rasilimali za umma kwa ajili ya maandili ya uchaguzi hadi pale kesi hiyo
itakaamuliwa.
Mwanzia amesema iwapo mahakama haitoingilia kati, IEBC itaendelea
kutumia rasilimali za umma kuendeleza michakato ambayo baadaye
itatajwa kuwa kinyume cha katiba.