Rais William Ruto ameweka wazi kwamba safari ya kubadilisha taifa la Kenya kuwa taifa lililoendelea itaanza rasmi siku ya Jumatatu wakati wa kikao cha baraza la mawaziri.
Akizungumza huko Gatundu kaunti ya Kiambu, rais Ruto amesema wakati wa kikao hicho baraza la mawaziri litaidhinisha hazina maalum ya miundo mbinu itakayohakikisha serikali inakusanya shilingi trilioni 5 za kutekeleza miradi ya kubadilisha taifa.
Rais Ruto aidha amesema huu sio wakati wa viongozi kujipigia debe kwa ajili ya kupata uungwaji mkono wakati wa uchaguzi mkuu ujao, badala yake wawajibike kuidhinisha maendeleo.
Story by Mimuh Mohamed



