Monday, 19January, 2026    7:24 am

Play Listen Live

Serikali kuu na zile za kaunti zahimizwa kuangazia maslahi ya watu wenye uatilifu.

Mwakilishi wa baraza la watu wanaoishi na ulemavu Emily Mwembe ameeleza haja ya kuzingatiwa kikamilifu haki za watu wenye uwezo maalum.

Akizungumza wakati maadhimisho ya siku ya watu wenye mahitaji maalum, katika shule ya wenye mahitaji maalum ya Kinango Mwembe amehimiza ikiwemo kuweka watafsiri wa lugha ya isha katika ofisi za umma.

Naye gavana wa kaunti ya Kwale Bi Fatuma Achani amewataka wakaazi kuwasajili watoto wenye mahitaji maalum ili wanufaike na miradi ya serikali inayowalenga, huku naibu gavana Chirema Kombo akiwasihi wazazi wenye uwezo maalum kutowaficha watoto hao.

 

Story by Kombo Mangale

Contact Details

Radio Kaya

P.O Box 172~80403
Kwale, Kenya

SMS  – 0702 885 885

General Enquiries
info@radiokaya.co.ke

© 2025 Radio Kaya. All rights reserved.