Zamzam Mohamed Akanusha Madai ya Ufujaji wa Fedha za NGAAF Mombasa
Mwakilishi wa kike kaunti ya Mombasa Bi Zam zam Mohamed, amekanusha
madai kwamba ofisi yake imejihusisha na ufujaji wa fedha za hazina ya
NGAAF.
Katika mahojiano na mwanahabari wetu, Zam zam amesema makundi
yaliokosa fedha za hazina hiyo katika awamu ya kwanza ya ugavi wa fedha
hizo, zimepata fursa katika awamu ya pili ya ugavi huo.
Zamzam amekosoa hatua ya baadhi ya watu kueneza propaganda kuhusiana
na ugavi wa fedha hizo, akisema watu hao hawana ufahamu kuhusu usimamizi
wa hazina hiyo.
Zam zam aidha amesema hatashurutishwa na wapinzani wake wa kisiasa
katika kutekeleza majukumu yake kwa wakaazi wa kaunti hiyo.